KIAMA CHA MAABARA BUBU CHATANGAZWA

Na Mwandishi wetu Dar es Salaam Wamiliki wa Maabara bubu nchini ambazo hazijasajiliwa wamepewa kipindi cha mwezi mmoja kuanzia leo hadi Aprili 30 wawe wamesajili Maabara zao ili kuepuka kufungiwa. Agizo hilo limetolewa mapema leo na Mkurugenzi wa Huduma za Tiba kutoka Wizara ya Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto Dkt. Grace Magembe